Loading...

ARSENAL, CHELSEA NGUVU SAWA



Santi Cazorla akipiga mpira uliomgonga mkononi beki wa Chelsea Gary Cahill wakati wa mechi ya leo.

Oscar wa Chelsea akikwaana na kipa wa Arsenal David Ospina wakati wa mtanange wa leo.

Kiungo wa Chelsea, Cesc Fabregas akizawadiwa kadi ya njano baada ya kujirusha akitafuta penalti.

ARSENAL na Chelsea leo zimeshindwa kutambiana katika mechi yao ya Ligi Kuu ya England iliyopigwa kwenye Uwanja wa Emirates jijini London. Mpaka mwisho wa dakika 90, Arsenal 0-0 Chelsea.

Kwa matokeo ya leo Chelsea wamefikisha pointi 77 wakiwa nafasi ya kwanza huku Arsenal wakiwa na pointi 67 katika nafasi ya tatu nyuma ya Manchester City.

VIKOSI:
Arsenal (4-2-3-1): Ospina, Bellerin, Mertesacker, Koscielny, Monreal, Coquelin (Welbeck 75), Cazorla, Ramsey, Ozil, Sanchez, Giroud (Walcott 82)

Waliokuwa benchi: Szczesny, Debuchy, Gibbs, Wilshere, Flamini

Chelsea (4-2-3-1): Courtois, Ivanovic, Cahill, Terry, Azpilicueta, Ramires, Matic, Willian (Cuadrado 90), Oscar (Drogba 46), Hazard, Fabregas (Zouma 90)

Waliokuwa benchi: Cech, Luis, Mikel, Loftus-Cheek

Kaseja kupandishwa tena kizimbani february 22



Kipa wa Yanga, Juma Kaseja kupitia kwa wakili wake, Samson Mbamba, jana amesomewa shtaka lake kwa mara ya kwanza la kuvunja mkataba kwenye Mahakama ya Kazi.

Kesi hiyo itaunguruma tena Februari 12 na Yanga wanataka Kaseja awalipe Sh340 milioni ikiwa ni ada ya usajili, ambayo ni Sh40 milioni pamoja na fidia ya Sh300 milioni, ambazo ni gharama za usumbufu wa kuvunja mkataba, kumhudumia na kutunza kiwango chake kwa kipindi chote alichokuwa Yanga.

Yanga inawakilishwa na mwanasheria wao, Frank Chacha, ambaye alifungua kesi hiyo Ijumaa iliyopita na ameliambia gazeti hili kuwa wamefikia uamuzi huo ili iwe fundisho kwa wachezaji wengine kuheshimu mikataba yao.

Kaseja aliingia kwenye mgogoro na uongozi wa Yanga baada ya Novemba 11 mwaka jana, kuandika barua ya kuvunja mkataba na klabu hiyo baada ya kukiuka makubaliano ya mkataba kati yao, akishinikiza kulipwa Sh20 milioni za usajili alizokuwa anaidai klabu hiyo.

Kaseja kupitia Kampuni ya Mbamba Advocate, iliandika barua ya kuvunja mkataba na klabu hiyo kwa kile ilichoeleza kuwa amekuwa akisugua benchi.

Pia, uongozi wa Yanga umekiuka makubaliano baina ya pande mbili ambazo hadi Januari mwaka jana walitakiwa kummalizia ada yake ya usajili Sh20 milioni, lakini hata hivyo, haikufanya hivyo hadi alipowasilisha barua ya kuvunja mkataba.

Akizungumza na gazeti hili, Wakili wa Kaseja, Samson Mbamba alisema: “Tutasimama kizimbani, hakuna shida, wala hatubabaishwi na lolote, naamini mteja wangu ana haki zote, mbivu na mbichi zitajulikana.”

Kwa upande wake, kipa huyo wa zamani wa Simba, Kaseja, alisema hana la kusema kwa sasa na kila kitu amekiacha mikononi mwa wakili wake

Kipa wa Yanga, Juma Kaseja kupitia kwa wakili wake, Samson Mbamba, jana amesomewa shtaka lake kwa mara ya kwanza la kuvunja mkataba kwenye Mahakama ya Kazi.

Kesi hiyo itaunguruma tena Februari 12 na Yanga wanataka Kaseja awalipe Sh340 milioni ikiwa ni ada ya usajili, ambayo ni Sh40 milioni pamoja na fidia ya Sh300 milioni, ambazo ni gharama za usumbufu wa kuvunja mkataba, kumhudumia na kutunza kiwango chake kwa kipindi chote alichokuwa Yanga.

Yanga inawakilishwa na mwanasheria wao, Frank Chacha, ambaye alifungua kesi hiyo Ijumaa iliyopita na ameliambia gazeti hili kuwa wamefikia uamuzi huo ili iwe fundisho kwa wachezaji wengine kuheshimu mikataba yao.

Kaseja aliingia kwenye mgogoro na uongozi wa Yanga baada ya Novemba 11 mwaka jana, kuandika barua ya kuvunja mkataba na klabu hiyo baada ya kukiuka makubaliano ya mkataba kati yao, akishinikiza kulipwa Sh20 milioni za usajili alizokuwa anaidai klabu hiyo.

Kaseja kupitia Kampuni ya Mbamba Advocate, iliandika barua ya kuvunja mkataba na klabu hiyo kwa kile ilichoeleza kuwa amekuwa akisugua benchi.

Pia, uongozi wa Yanga umekiuka makubaliano baina ya pande mbili ambazo hadi Januari mwaka jana walitakiwa kummalizia ada yake ya usajili Sh20 milioni, lakini hata hivyo, haikufanya hivyo hadi alipowasilisha barua ya kuvunja mkataba.

Akizungumza na gazeti hili, Wakili wa Kaseja, Samson Mbamba alisema: “Tutasimama kizimbani, hakuna shida, wala hatubabaishwi na lolote, naamini mteja wangu ana haki zote, mbivu na mbichi zitajulikana.”

Kwa upande wake, kipa huyo wa zamani wa Simba, Kaseja, alisema hana la kusema kwa sasa na kila kitu amekiacha mikononi mwa wakili wake

YANGA KUMPANDISHA KIZIMBANI JUMA KASEJA



Baada ya Uongozi wa Klabu ya Yanga kutangaza kuachana na aliekuwa mlindamlango wake Juma Kaseja na baadae kumfungulia mashtaka katika Mahakama ya kazi , hatimaye mlind amlango huyo sasa anatarajia kusomewa mashtaka yanayomkabili February 12 mwaka huu.
Hatua hiyo ilikuja kufuatia Kaseja kudai alipwe fedha zake za usajili zilizokuwa zimesalia na kutaka kuvunja mkataba wake , lakini baadae Klabu hiyo ilimuingizia pesa hizo katika akaunti yake bila kumpa taarifa na kupelekea kuwepo kwa mgogoro baina ya pande hizo mbili.
Mkuu wa Idara ya Sheria ya Klabu hiyo FRANK CHACHA ameiambia mtandao huu kwamba wamepokea samasi inayomtaka mlindamlango huyo kufika Mahakamani hapo kwa ajili ya kesi hiyo
Older Posts
© Copyright Bongo Mirror | Designed By BONGOJAMII.COM
Back To Top