Loading...

MWANAUME ALIYEOTA MATITI!!!

BAGAMOYO
Mkazi wa kijiji cha Magomeni Wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani, Khamisi Tanga (46), ameota matiti katika hali isiyo ya kawaida ikidaiwa imesababishwa na kutumia dawa za kupunguza makali ya Ukimwi ARV’S.

SOMA HII,, DIAMOND PLATINUMZ, ZARI NDANI YA POWER BREAKFAST NA CLOUDS 360 KESHO





HOT NEWS,,UNENE WAMTESA SELENA GOMEZ






Staa wa muziki wa Pop, Selena Gomez.

NEW YORK, MAREKANI

WAZUNGU bwana! Staa wa muzikiwa Pop, Selena Gomez ameendelea kuteswa na unene ulioongezeka kwa muda mfupi huku mitandao ya kijamii ikimshambulia. Staa huyo aliyekuwa mpenzi wa staa mwenzake wa muziki, Justin Bieber kupitia ukurasa wake wa Instagram, mashabiki wake wengi wameonekana kukerwa na unene huo jambo linalomnyima usingizi staa huyo.



Kabla hajaongezeka unene.

“Selena anachukizwa na watu wanaoongelea unene wake na hilo linamuweka katika wakati mgumu wa kumsikia kila mtu akimuongelea, anaumia sana,” alisema shabiki mmoja wa staa huyo.

UNAPOMSIFU MPEZI WAKO KWA UJUZI WAKE, HUJIULIZI KAUTOA WAPI..!!






Kwetu tunaamini mchawi aliyekubuhu, ni yule aliyeuwa watu wengi zaidi. Au hata ukimuona dereva anakimbiza gari barabarani unaamini ana uzoefu wa udereva wa mda mrefu na atakuwa ameshawahi kuendesha magari mbali mbali.

Sasa linapokuja swala la mahusiano, ninaona watu wanalalamika kuhusu ujuzi wa wenzi wao. Ingekuwa mimi, endapo mwenzi wangu angekuwa na kiwango kidogo cha ujuzi kwenye maswala ya chumbani, lingekuwa jambo la furaha na kheri.
Pale unapotaka mpenzi wako awe na ujuzi wa PhD katika maswala ya chumbani, wewe unataka awe amejifunzia wapi? Kama unataka mjuzi, nenda kachukue Changu doa ambaye anajua michezo yote...
Dada zetu waliofunzwa wakatulia, na kaka zetu au wadogo zetu waliofunzwa wakatulia technically watakuwa na ujuzi mdogo na over the time katika maisha yao ya mahusiano (ndoa) wataweza kujifunza na kuimprove.

Ukimpata yule anayekupeleka puta, inabidi ukae chini na ujiulize atakuwa amewapitia au amepitiwa na wangapi mpaka akapata utaaalam huo?

BARUA NZITO: WASTARA AOMBA RADHI‭, WAMUONYA KU‬BADILI MWELELEKEO !‬




Wastara Juma

KWAKO mwanamke unayejua kuuvaa vyema uhusika katika sinema za Kibongo, Wastara Juma. Za siku nyingi? Uko poa mama!&ke?

Ukitaka kujua afya yangu mimi ni mzima wa afya, naendelea na mishemishe zangu za kila siku kuhakikisha mkono unakwenda kinywani. Nimekukumbuka hapa leo maana ni kitambo kidogo hatujaonana. Nikaona ni vizuri kukuandikia barua.

Dhumuni la barua hii ni kwanza kutaka kukukumbusha juu ya heshima niliyokuwa nakupa. Nilikuwa nakuheshimu kama mama wa watoto wawili, mtu mzima mwenye busara za kutosha.

Kwa levo ya heshima niliyokuwa nakupa, sikuwahi kuwa na shaka kwamba labda kuna siku unaweza ukabadilika. Niliamini kadiri siku zilivyozidi kusonga ndivyo busara zaidi zingeendelea kujaa katika kichwa chako.

Nilikuheshimu kama mama jasiri sana. Historia ya maisha yako inaonesha umepitia mitihani mingi, kwa namna ambavyo umepambana na kuvuka viunzi hivyo, hakuna ambaye anaweza kuwa na shaka na wewe zaidi ya kukupongeza na kukuona ni mfano wa kuigwa.

Ulipambana sana kutetea uhai wa mumeo hadi pale Mungu alipomchukua. Nikwambie Watanzania walikupa heshima ya juu. Mimi mwenyewe nilikuheshimu sana. Sikuwahi kutarajia kama siku moja unaweza kushusha heshima yako kirahisi kama wafanyavyo baadhi ya wasanii.

Sikuwahi kuwaza kama kuna siku ninaweza kukuona umevaa mavazi ya ajabu kama wafanyavyo baadhi ya wenzako, achilia mbali ulevi wa kupindukia.

Niliamini wewe ndiye mtu wa kukemea wenzako wanaotoka nje ya mstari wa kujiheshimu.

Licha ya kukuheshimu huko kwa muda mrefu, juzikati ulifanya tukio ambalo nilipoliona, akili yangu ilishindwa kuamini kama ni wewe yule ninayekuheshimu. Nazungumzia matusi mazito uliyoyaporomosha kwenye mtandao wa Instagram.

Ulimtukana mmoja wa mashabiki wako matusi mazito ya nguoni. Najua kabisa kwamba alikuudhi na kama binadamu unakasirika, lakini siku zote kabla ya kufanya jambo lolote lazima kwanza uangalie nafasi yako katika jamii.

Huwezi kumuona chizi anakutukana eti na wewe ukamtukana ili kumkomoa. Mwenye busara na hekima, akitukanwa na chizi, hukaa kimya na mwisho wa siku watu hubaini nani ni chizi!

Kwa matusi uliyomlipizia yule shabiki wako, waungwana walikujadili wewe uliyejibu badala ya shabiki wako.

Walikuona hukutumia busara. Kwa nafasi yako katika jamii, ukisema umjibu kila atakayekutukana, utawatukana wangapi? Jamii nayo itakuelewaje?

Nikuambie tu dada yangu hukufanya kitu kizuri hata kidogo, wewe ni staa mwenye heshima kubwa, huwezi kutukana matusi mazito kiasi kile hadharani, tena kwenye akaunti yako ambayo unaitumia kufanya biashara mbalimbali.

Binafsi tangu siku ile niliposoma posti yako nilijisikia vibaya, sikutegemea. Ningekushauri, ili kurejesha heshima yako, omba radhi na kubadilika. Kwa leo ni hayo tu.

Wasalaam

FAMILIA WASHAMBULIA DIAMOND ,,,,,TUNASHAKA NA MIMBA YA ZARI



SHAKA! Familia ya ‘President’ wa Kruu ya Wasafi, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ imeamua kuweka kikao kummbana staa huyo aweke wazi kama ni kweli ana uhakika mimba aliyonayo mjasiriamali Zarinah Hassan ‘Zari’ ni ya kwake au magumashi, Risasi Mchanganyiko linakupa mchapo kamili.

Diamond Platnumz akibusu tumbo la mpenzi wake Zari.

TUJIUNGE NA CHANZO

Kwa mujibu wa chanzo kilicho karibu na familia ya staa huyo, ndugu wa karibu akiwemo mama, binamu yake Romy Jons, wajomba zake, mameneja na marafiki wa karibu wa familia, waliamua kuweka kikao hicho usiku hivi karibuni ili Diamond athibitishe kama kweli kiumbe kinachoripotiwa kuwa ni cha kwake magazetini ni chake kweli.

Diamond akiwa katika pozi na mpenzi wake Zari.

“Ndugu walichachamaa, walitaka kujua kama kweli mimba inamhusu Diamond au ni magumashi ya kiki za vyombo vya habari.

“Kwenye hicho kikao walimualika na Diamond mwenyewe ili aweze kufunguka kama ana uhakika kweli mimba ni yake,” kilisema chanzo hicho

WALITAKA ATOE MSIMAMO

“Mbali na kutaka kujua kama mimba ni yake, walitaka pia kujua ana msimamo gani na Zari maana kila kukicha wanasikia mambo tofauti katika mitandao na vyombo vya habari,’’ kilisema chanzo hicho.

SABABU ZAZIDI KUANIKWA

Chanzo hicho kilipobanwa na mwanahabari wetu kuhusiana na sababu zilizowafanya ndugu wa Diamond watilie shaka mimba hiyo, kilisema ni kauli ambazo ziliwahi kusemwa na aliyekuwa mpenzi wake Penniel Mungilwa ‘Penny’ na aliyekuwa mume wa Zari, Ivan Semwanga.

“Walishitushwa na kauli ambayo aliwahi kuitoa Penny kwamba Diamond hana uwezo wa kumpa mwanamke mimba lakini kama hiyo haitoshi, waliitafakari kauli ya mume wa Zari ambaye alidai Zari hawezi kumzalia Diamond ndiyo maana wakataka wapate uhakika,” kilisema chanzo hicho.

MUAFAKA WA KIKAO

Chanzo hicho kikizidi kumwaga ubuyu mbele ya kinasa sauti cha Risasi Mchanganyiko kwamba, baada ya Diamond kubanwa na nduguze, alithibitisha kuwa Zari ndiyo kila kitu kwake kwa sasa, hivyo wasiwe na shaka yoyote juu ya kiumbe kinachotarajiwa kuzaliwa.

“Diamond aliwahakikishia kwamba mzigo ni wake, na msimamo wake ni kufika katika hatua ya ndoa Mungu akijalia.

KUMVISHA PETE

“Kuonesha yupo serious baada ya Diamond kuwatoa hofu ndugu zake, alisema atafanya sapraiz siku ya Mei Mosi katika shoo ya mrembo huyo, All White Party itakayofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar,” kilisema chanzo hicho na kudokeza kuwa Diamond atamvisha pete mrembo huyo.



DIAMOND AFUNGUKA

Ili kuweza kupata ukweli, mwanahabari wetu alimtafuta Diamond ili aweze kuweka wazi juu ya kikao hicho na kama ni kweli anatarajia kumvisha pete Zari. Diamond alifunguka:

“Yeah ni kweli ndugu zangu walikuwa na shaka lakini nimewahakikishia kwamba kiumbe kilichomo tumboni mwa Zari ni mali yangu, kuhusu kumvisha pete ni mapema kidogo kulizungumzia lakini watu wahudhurie kwa wingi katika shoo ya Zari White Party Ijumaa hii pale Mlimani City kwani nimeandaa sapraizi nyingi sana.

“Mei Mosi itakuwa ni siku ya kihistoria sana kwake kwani kuna mambo muhimu mengi natarajia kumfanyia mpenzi wangu Zari, watu watajua rasmi nia yangu kwa Zari maana ni mwanamke ambaye ameamua kujitoa kwa ajili yangu, hivyo sina budi kumuonesha upendo stahiki, nitafanya kila linalowezekana kumuonyesha namna gani nampenda.”

SHOO YA KIHISTORIA

Kwenye shoo hiyo ya Zari, watu mbalimbali mashuhuri wanatarajiwa kuhudhuria akiwemo dairekta mkubwa Afrika, Godfather wa Afrika Kusini na Top Ten ya Washiriki wa Shindano la Big Brother ‘Hot Shot’ 2014.

FANYA HAYA..!! UNAPOTOKEA KUMPENDA MTU ALIYE NA MPENZI WAKE






Tumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye ametuwezesha kuonana tena wiki hii tukiwa wazima. Lakini pia tumshukuru kwa kutuletea kitu kinachoitwa mapenzi.
Mapenzi yamekuwa yakichukua nafasi kubwa sana katika maisha yetu ya kila siku na yamekuwa yakichangia kwa kiasi kikubwa furaha kwa kila mtu.
Kama huamini, angalia wale waliotokea kupenda na wao wakapendwa, utabaini nyuso zao zimetawaliwa na furaha isiyo na kifani. Lakini mapenzi hayo hayo yamekuwa ni chanzo cha vilio kwa baadhi ya watu.
Mpenzi msomaji wangu, kupenda hakuna macho! Moyo ukishapenda hausikii la kuambiwa. Katika hili ndiyo maana unaweza kumuona mwanaume kazimika kwa demu ambaye hawaendani kabisa lakini moyo wake ndiyo umeshapenda.
Ilishawahi kutokea msichana akampenda kijana mmoja ambaye ni fukara kupita maelezo. Yeye akawa ndiyo anamhudumia kwa kila kitu. Akamfanyia mpango wa ajira na mwisho wake wakafunga ndoa.
Sasa hivi wanaishi maisha ya furaha na amani. Wamegeuka mfano wa kuigwa kwa jinsi wanavyopendana lakini huko nyuma msichana huyo alikuwa akichekwa kwa kutoa penzi kwa mwanaume asiye na mbele wala nyuma.
Hayo ndiyo mapenzi jamani! Lakini pia katika kufurukuta kumtafuta mpenzi wa kuwa naye maishani, mwanaume anaweza kujikuta unaangukia kwa demu ambaye tayari ana mpenzi wake.
Moyo wako unakuambia yeye ndiye mtu sahihi katika maisha yako lakini tayari ana mtu wake, unafanyaje?
Utapambana kuhakikisha unapata kile ambacho moyo wako umekipenda au utakubaliana na ukweli kwamba huwezi kuwa naye kwa kuwa ana mtu wake? Inapofikia hatua hiyo unaweza kujikuta upo njia panda hasa pale ambapo huyo mwenye mtu wake naye anaonesha kuwa na chembechembe za mapenzi kwako. Kuna mambo kadhaa ya kukusaidia kukabiliana na hali hii.
Chunguza Tumia muda wako mwingi kuchunguza juu ya uhusiano wake. Uhusiano wao umesimama na wanaonekana ni watu wenye ‘future’? Nasema hivyo kwa sababu, yawezekana uhusiano wa huyo uliyetokea kumpenda ni wa kuzuga tu na huenda wewe ndiye mwenye ‘future’ naye. Ndiyo maana nikasema chunguza uhusiano wake kwanza.
Usitafute uadui Baada ya kuchunguza, ukibaini kwamba uhusiano wao hauko ‘siriasi’, vuta subira, lolote linaweza kutokea na likaufurahisha moyo wako. Lakini kama utaona ni watu walio siriasi na wanaelekea kuoana, usitafute uadui bure, kaa pembeni.
Una nafasi kwake? Sawa umetokea kumpenda msichana aliye na mtu wake, umeshawahi kujiuliza kama una nafasi ndani ya moyo wake? Anaonesha dalili fulani za kukupenda kama unavyompenda na ni mtu anayeonesha kukumisi anapokuwa mbali na wewe? Utakapobaini una nafasi kwake, uamuzi wa kumpotezea hautakuwa na nafasi.
Ni rahisi kubadili uamuzi wake? Unadhani huyo uliyetokea kumpenda anaweza kubadili maamuzi ya kumuacha huyo aliyenaye kama kweli hawana ‘future’? Utagundua hilo kwa kuongea naye na kumsikia kama anaweza kufanya maamuzi hayo ili awe na wewe.
Pingana na moyo wako Ifike wakati upingane na moyo wako. Unajua moyo wako kukuambia kuwa unataka kuwa na uhusiano na demu ambaye tayari ana mpenzi wake wakati mwingine utakuwa unakupotosha.
Kwa hiyo ukiona vipi, pingana nao. Acha kumng’ang’ania msichana mwenye mpenzi wake licha ya ukweli kwamba, huenda wewe ndiye mwenye nafasi ya kuwa mume wake na siyo huyo aliye naye.
Urafiki ni poa? Umempenda sana na hauko tayari kumkosa katika maisha yako lakini imetokea kwamba tayari yuko na mtu na umebaini huna nafasi kwake kabisa? Usiumie, omba angalau urafiki. Siyo urafiki wa kivile sana ila angalau pale unapotaka kusikia sauti yake kwa kumsalimia tu, upate nafasi hiyo.
Usiumie, yupo mwingine Haina haja ya kujitafutia vidonda vya tumbo bure kwa kuwa tu umebaini uliyetokea kumpenda tayari ana mtu. Chukulia ni hali ya kawaida, mademu wazuri ambao wanaishi singo wapo kibao huko mtaani, ni suala la wewe kutulia tu. Amini yupo mwingine ambaye atayafanya maisha yako yawe ya furaha.
Naomba nihitimishe kwa kusema kwamba, unapotokea kumpenda mtu fulani, pambana kuhakikisha unampata kwa sababu ukimkosa maisha yako yanaweza kuwa gizani. Ila pale utakapoona uwezekano wa kuwa naye haupo, usilazimishe ndugu yangu. Kumbuka haya ni maisha tu!

WEMA ADAIWA KUTIBUA NDOA YA PETIT MAN






Hatimaye lile sekeseke la ndoa ya meneja wa wasanii wa Bongo Fleva wanaosimamiwa na Kampuni ya Endless Fame, Petit Man na mdogo wa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Esma Platnumz limemdondokea Wema Isaac Sepetu anayedaiwa kuitibua kiasi cha kuwatenganisha na kila mmoja kuchukua hamsini zake.

Mdogo wa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Esma Platnumz.

Habari kutoka chanzo chetu zilidai kwamba, Wema amehusika kwa asilimia kubwa kutibua ndoa hiyo kwani amekuwa akimtafutia mademu Petit Man, jambo ambalo Esma alilishtukia na kuamua kumbwatukia Wema kwa kuandika maneno makali kwenye mitandao ya kijamii.

“Kwa taarifa yenu Esma anamlalamikia Wema kuwa anamfanya mumewe kuwa mhuni kiasi kwamba anachukua mademu, tena marafiki zake na hata akimuuliza Petit Man anajifanya hao ni mashoga wa Wema.“Anapomkomalia, mara kadhaa umekuwa ukizuka ugomvi mkubwa na Petit Man anahama nyumbani kwake na kukimbilia kwa Wema,” kilisema chanzo chetu.Baada ya kunyetishiwa ‘infomesheni’ hizo, gazeti hili liliingia kazini kusaka ukweli wa mambo yanayodaiwa.

Wema Isaac Sepetu.

Lilianzia kwa Esma, alipopatikana alisema ni kweli hivi karibuni aliandika ujumbe kwenye Mtandao wa Instagram, ingawa kwenye maelezo yake hakumtaja mtu bali aliandika kwa hisia kama binadamu mwingine anavyoweza kuandika.

“Nani anasema nimemtukana mtu? Niliandika mambo ambayo nilijisikia mwenyewe lakini sikumtaja wala kumlenga mtu yeyote, kama kuna mtu alikwazika basi atakuwa anajichanganya mwenyewe.“Mimi sina tatizo na Wema na mambo ya familia yangu siwezi kumwambia kila mtu hivyo kama kuna ugomvi kati yangu na mume wangu hayo ni mambo ya familia yetu,” alisema Esma.

Kwa upande wake Wema alifunguka kwamba hajawahi kuongea jambo na Esma na kama kuna kitu aliandika kwenye ‘peji’ yake yeye hakuona.Alisema anachokumbuka ni kwamba aliongea naye (Esma) akiwa Hospitali ya Aga Khan Aghakan, Dar.

Esma Platnumz na Petit Man siku ya ndoa yao.


“Huwa siongei na Esma mara kwa mara kwani sina sababu sana ya kuwa naye kwa kuwa si mume wala bwana’ngu.
“Pia sijawahi kukwaruzana naye, sasa kama kuna kitu alisema, mimi namtafutia wanawake mumewe basi atakuwa anakosea kabisa,” alisema Wema.

BREAKING NEWZ.... MKE MTARAJIWA APASUA JIPU



Erick evarist
KWELI! Baada ya mitandao mbalimbali kuripoti habari zinazokinzana juu ya tukio la bwana harusi mtarajiwa aliyetajwa kwa jina la Stephano kunaswa kwenye tukio la ujambazi muda mfupi baada ya kumvisha pete ya uchumba mpenzi wake, Happy Merere, bi. Harusi huyo mtarajiwa ameibuka na kuanika ukweli wa mambo, Risasi Jumamosi lina full stori.

Stephano akiwa na mpenzi wake, Happy Merere baada ya kumvisha pete ya uchumba.

Stephano na wenzake watatu walikamatwa Aprili 21, mwaka huu maeneo ya Red Cross jijini Dar akidaiwa kuhusika katika tukio la kumpora fedha Mzungu mmoja raia wa kigeni pale Kinondoni, Dar.
Kwenye tukio hilo, watuhumiwa hao, akiwemo Stephano au mume mtarajiwa wa Happy waliwekwa chini ya ulinzi na jeshi la polisi.

MITANDAO YAANZA
Baada ya tukio hilo kuthibitishwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam na watuhumiwa Salum Mtamwa, Alex Makunga, Mohammed Ally na Stephano Kikindi kushikiliwa kwa uchunguzi zaidi, watu walianza kuripoti tofauti katika mitandao ya kijamii.Kuna ambao walidai watuhumiwa hao ni majambazi kwa vile walikutwa na bunduki mbili lakini kuna wengine walidai ni vibaka kwa kuwa hawakukutwa na silaha yoyote.

WENGINE WANADAI NDIYO TABIA YAKE
Wadau wengine kwenye mitandao ya kijamii walijiongeza kwa kudai mtuhumiwa ambaye ni mume mtarajiwa wa Happy wanamjua kwamba anajihusisha na ishu za udokozi hivyo tukio hilo si la kwanza kumtokea.

MKE MTARAJIWA AIBUKA
Risasi Jumamosi lilibahatika kuzungumza na Happy ambaye awali alianza kukanusha taarifa ambazo zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii na kudai nyingi hazina ukweli wowote, alisema:
“Wanajiandikia tu mitandaoni, hakuna ukweli wowote. Eti wanasema mchumba‘angu amekutwa na bunduki mbili wakati taarifa nilizozikuta pale Polisi Central zinasema hawakuwa na silaha.”

ASEMA SI JAMBAZI!
“Wala mchumba‘angu hakuwa jambazi kama watu walivyokuwa wanasema mitandaoni, jalada nililolikuta polisi lilikuwa limeandikwa UNYANG’ANYI na si ujambazi kama wengi walivyokuwa wanavumisha, mimi nimekwenda mwenyewe polisi nikaoneshwa.”

Stephano anayetuhumiwa kwa ujambazi.

KUMBE WAMEJUANA KITAMBO
Katika aya nyingine, Happy alizungumzia uhusiano wake na mumewe mtarajiwa huyo na kusema walifahamiana miaka mingi lakini hawakuwa wakiishi pamoja.“Mimi nimejuana naye miaka mingi iliyopita lakini hatukuwa tukiishi pamoja, yeye anakaa Dar, mimi nipo nyumbani kwa wazazi wangu, Iringa.”

NI MTU WA KUSAFIRI
“Hata hivyo, mimi mwenyewe nyumbani nilikuwa sikai sana, nilikuwa mtu wa kusafiri maana nina biashara zangu, hata yeye tulikuwa tunaonana mara chache.”

KAZI YA MTARAJIWA WAKE
“Tangu nimemjua mtarajiwa wangu alikuwa anafanya kazi ya ufundi wa magari pamoja na udalali wa magari, sikuwahi kusikia wala kumuona anajihusisha na wizi wa namna yoyote. Nashangaa eti watu wanadai ni mzoefu wa matukio ya wizi.”

ADAI NI MARAFIKI
“Wale watu aliokamatwa nao mchumba wangu ni marafiki zake, sasa huenda alijikuta amejumlishwa kwenye tukio ambalo halimhusu. Watu wanazungumza tu pasipo kuwa na ushahidi wowote, mimi mchumba wangu namjua sijawahi kumuona na viashiria vyovyote vya wizi,” alisema Happy.

Stephano na wenzake waliponaswa kwenye tukio hilo.


WAZAZI WACHANGANYIKIWA
Happy alizidi kuweka wazi kuwa, ameumizwa na tukio hilo kwani limewagusa wazazi wake kiasi cha kuwafanya wachanganyikiwe.“Huwezi amini, wazazi wamechanganyikiwa, wanaelezwa vitu vya uongo kuhusu mtarajiwa wangu inaniuma kwa sababu yanayoongelewa kwenye mitandao hayana ukweli, ila ngoja tusubiri vyombo vya sheria vifanye kazi yake na wote waliosema uongo wataumbuka,” alisema Happy.

TUKIO LA PETE
Februari, mwaka huu, Happy alivishwa pete na mchumba wake huyo nyumbani kwao Iringa ambapo mipango ikienda sawa, wawili hao wanatarajiwa kufunga ndoa hapo baadaye mwaka huu (Mungu akipenda).

NAY WA MITEGO, SHAMSA MKE NA MUME!




Musa Mateja

Mara baada ya kuelezwa kwamba wapo kwenye uhusiano wa kimapenzi huku wenyewe wakidanganya wana ‘projekti’, hatimaye majirani wamefichua kuwa mwigizaji Shamsa Ford na mwanamuziki Emmanuel Elibariki ‘Nay’, sasa wanaishi kama mke na mume.

Mwigizaji Shamsa Ford na mwanamuziki Emmanuel Elibariki ‘Nay’ wakizungumza jambo.

Baada ya kutonywa ‘mchapo’ huo, gazeti hili liliwadamkia nyumbani kwa Nay maeneo ya Kimara-Korogwe jijini Dar na kumkuta Shamsa akiwa na kanga moja.Mwanahabari wetu, baada ya kufika nyumbani hapo mishale ya asubuhi alikuwa bega kwa bega kuwafuatilia ambapo alifanikiwa kugundua kwamba wawili hao sasa wanaishi kama mume na mke.

Habari zilizopatikana zilidai kwamba, kwa sasa Shamsa hana muda mwingi wa kukaa nyumbani kwake kwani asilimia tisini kama si mia moja kabisa, anautumia kukaa na Nay nyumbani hapo.Mara kadhaa mwandishi wetu amekuwa akifika nyumbani hapo na kumkuta Shamsa akipika na kupakua huku akiwa na kanga moja huku wenyewe wakiitana mke na mume na kuoneshana mahaba motomoto.

...Wakipozi kimahaba.

“Kwani tatizo lipo wapi? Siwezi kufanya siri tena, sisi tupo kwenye uhusiano wa kimapenzi kama unavyotuona, nimeamua kumchagua Nay kwa kuwa anajua kupenda na kuthamini,” alisema Shamsa alipohojiwa na paparazi wetu.
Alipoulizwa Nay kulikoni ‘kumficha’ Shamsa nyumbani kwake, alifunguka:

“Yeah! Kwa sasa hakuna project tena, hapa ni mapenzi kwa kwenda mbele, sipendi kuwazungumzia wengine, napenda kuangalia uhusiano wangu upo vipi kwa sasa, ninampenda Shamsa.”

...Wakipata msosi.

Nay na Shamsa walianza uhusiano huo mara baada ya mwanamuziki huyo kudai kwamba alimnasa mpenzi wake, Siwema akiwa na mwanaume ndani ya sita kwa sita hivyo kuamua kuachana naye moja kwa moja na kujikuta akiangukia kwa mwigizaji huyo.

A WONDER STORY CLICK TO READ.........'Right' Reasons to Get Married





This is a very important question and sadly, I don't think many people actually ask themselves this question until it's too late.

Lets talk about the "right" reasons to get married:
You share common beliefs about life and marriage.
You are capable of working out differences respectfully.
You can respect each other even when you disagree.
You accept each other for who you are and are willing to support them towards their goals.
You love each other without conditions (having the right weight, education, quid pro quo.)
You feel loved and supported by their family and friends.
You have each other's back and are willing to protect and defend each other when needed.
You are not expecting the other person to "make you happy."
You are interested in sharing and building a life together.
You can tell the person you love what you need and want without manipulation or guilt.
You know you can be vulnerable with each other without judgment or criticism.

If you are uncomfortable about talking about money, sex, time, goals and family concerns with your potential spouse, before you get married.... the situation will not improve once you are married.


This is just something to keep in mind. Get into healthy conversation habits before you make the commitment official. This practice will greatly improve the quality and longevity of your relationship.

Remember, just because you love someone doesn’t mean that you have to marry them. Love is important in marriage, but compatibility is a requirement in order for two people to live a long healthy life together.

I’ve experienced many couples who still loved each other, but love was not enough to remove all of the things that were left unsaid or hidden from their spouse.

If you can’t discuss important issues within your partnership, how will the two of you survive anything and everything that comes your way?

In the next episode, we will discuss the wrong reasons to get married.

If you are avoiding having a difficult conversation with someone and would like to know where to start, you can check out my online course entitled,

AMANDA ACHARUKIWA KISA NGOMA


MWANDISHI WETU

MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Tamrina Poshi ‘Amanda’ amefunguka kuwa baada ya kukanusha kuwa hana ugonjwa wa Ukimwi, mpenzi wake amemcharukia kweli akihoji kwa nini akanushe kama hana?

Mwigizaji wa sinema za Kibongo, Tamrina Poshi ‘Amanda’.

Akizungumzia tukio hilo, Amanda alisema baada ya gazeti la Ijumaa la wiki iliyopita kuripoti akimchana shabiki aitwaye Joel ambaye aliandika mtandaoni kuwa mwigizaji huyo anatumia vidonge vya ARV ili kuongeza nguvu za kuishi, ndipo mchumba wake akacharuka.

“Baby alicharuka kweli akadhani labda pengine ni kweli wakati mimi nimepima na majibu yangu ni mazuri, nilimuelewesha kwamba nilimchamba yule shabiki ambaye aliropoka tu bila ushahidi, nashukuru alinielewa na sasa tuko poa,” alisema Amanda.

AJALI YA MOTO KICHANGA CHAOKOA FAMILIA!

KICHANGA kinachokadiriwa kuwa na umri wa miezi nane, wiki iliyopita kiliiokoa familia yake kuteketea kwa moto, baada ya kuamka usiku na kulilia kunyonya, kitendo kilichomshtua mama yake aliyebaini nyumba yao ilikuwa ikiungua, huko Kibamba Lungwe jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya nyumba iliyoungua.
Akisimulia tukio hilo, mama wa kichanga hicho, Asha Mohamed, alisema alishtuka baada ya mtoto kuanza kulia akitaka kunyonya, alipoamka ndipo akaona mwanga mkali juu ya paa, hali iliyomlazimu kuamka na kwenda kumgongea Abuu ili kutafuta njia ya kutoka,” alisema mama huyo akiongeza kuwa sebuleni, moto ulikuwa umetapakaa.

Kijana Abuu Masoud (15), baada ya kuamshwa, alionyesha ujasiri na upendo mkubwa kwa kujitoa mhanga kuwasaidia wadogo zake watatu waliokuwa wamelala katika moja ya vyumba vya nyumba hiyo.
Baada ya kuingia katika chumba hicho, alifanikiwa kumtoa mtoto mmoja.
Watoto walionusulika kuteketea kwa moto.
“Nilipofungua mlango wa sebuleni nikaona moto na moshi mwingi sana, roho iliniuma sana kwani chumba cha pili kulikuwa na wadogo zangu watatu wamelala, nikaamua kuvaa ujasiri na kujitosa katika chumba kile na kufanikiwa kutoka na mtoto mmoja, wakabaki wawili,
baada ya kurudi ndani nikapata wazo la kuzima Mean switch, nilipoenda kuishika ikaniangukia kichwani kwani ilikuwa imeshaungua, ndiyo nikaungua na kushindwa kuwatoa waliobakia, ingawa baadaye kuna msamaria mwema mmoja alijitokeza na kuja kubomoa mlango na kuwatoa wengine,” alisema kijana huyo.
....Kitanda walichokuwa wamelala.
Mama wa mtoto mchanga alifanikiwa kutoka pasipo kudhurika.
Aidha baba mwenye nyumba hiyo, Khalfani Maketemo, ambaye wakati nyumba yake inaungua yeye na mkewe walikuwa hospitali alikokuwa amelazwa, anadai chanzo cha moto huo ni shoti iliyoanzia kwenye bati na anaamini ni kutokana na kuunganishwa vibaya kwa waya unaopitisha umeme kutoka kwenye nguzo kwenda kwenye nyumba.
Wakizungumza na mwandishi wetu baadhi ya majirani walisema; “Uunganishwaji wa umeme ni wa kubabaisha, waya unagusana na bati jambo ambalo ni hatari kama waya utachubuka na mvua kunyesha’’.Familia hiyo kwa sasa haina sehemu ya kujisitiri nyumba nzima imeteketea.
Older Posts
© Copyright Bongo Mirror | Designed By BONGOJAMII.COM
Back To Top