Loading...

click to view all event of today jamaica olympic....matukio yote ya riadhaaa




ZARI AONYWA NA DACTARI VIATU VIREFU NA UJAUZITO NI SHIDAH




MWANDISHI WETU

UBAVU wa Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari’ ameonywa kuacha viatu virefu kutokana na ujauzito alionao.
Kwa mujibu wa daktari mmoja ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazetini, alisema kama anataka kujifungua salama basi ahakikishe anaachana na suala la kuvaa viatu virefu kwa wakati huu ambao ni mjamzito.

Ubavu wa Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari’.

“Kama anajipenda na anampenda mwanaye ajaye, anapaswa kuachana na mambo ya viatu virefu kwa sasa hadi pale atakapojifungua,” alisema daktari huyo.Katika picha za hivi karibuni ambazo Zari amepigwa, tumbo lake linaonesha kwamba tayari mimba yake ni kubwa na yuko mbioni kuelekea kujifungua.

WEMA ADAIWA KUTIBUA NDOA YA PETIT MAN






Hatimaye lile sekeseke la ndoa ya meneja wa wasanii wa Bongo Fleva wanaosimamiwa na Kampuni ya Endless Fame, Petit Man na mdogo wa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Esma Platnumz limemdondokea Wema Isaac Sepetu anayedaiwa kuitibua kiasi cha kuwatenganisha na kila mmoja kuchukua hamsini zake.

Mdogo wa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Esma Platnumz.

Habari kutoka chanzo chetu zilidai kwamba, Wema amehusika kwa asilimia kubwa kutibua ndoa hiyo kwani amekuwa akimtafutia mademu Petit Man, jambo ambalo Esma alilishtukia na kuamua kumbwatukia Wema kwa kuandika maneno makali kwenye mitandao ya kijamii.

“Kwa taarifa yenu Esma anamlalamikia Wema kuwa anamfanya mumewe kuwa mhuni kiasi kwamba anachukua mademu, tena marafiki zake na hata akimuuliza Petit Man anajifanya hao ni mashoga wa Wema.“Anapomkomalia, mara kadhaa umekuwa ukizuka ugomvi mkubwa na Petit Man anahama nyumbani kwake na kukimbilia kwa Wema,” kilisema chanzo chetu.Baada ya kunyetishiwa ‘infomesheni’ hizo, gazeti hili liliingia kazini kusaka ukweli wa mambo yanayodaiwa.

Wema Isaac Sepetu.

Lilianzia kwa Esma, alipopatikana alisema ni kweli hivi karibuni aliandika ujumbe kwenye Mtandao wa Instagram, ingawa kwenye maelezo yake hakumtaja mtu bali aliandika kwa hisia kama binadamu mwingine anavyoweza kuandika.

“Nani anasema nimemtukana mtu? Niliandika mambo ambayo nilijisikia mwenyewe lakini sikumtaja wala kumlenga mtu yeyote, kama kuna mtu alikwazika basi atakuwa anajichanganya mwenyewe.“Mimi sina tatizo na Wema na mambo ya familia yangu siwezi kumwambia kila mtu hivyo kama kuna ugomvi kati yangu na mume wangu hayo ni mambo ya familia yetu,” alisema Esma.

Kwa upande wake Wema alifunguka kwamba hajawahi kuongea jambo na Esma na kama kuna kitu aliandika kwenye ‘peji’ yake yeye hakuona.Alisema anachokumbuka ni kwamba aliongea naye (Esma) akiwa Hospitali ya Aga Khan Aghakan, Dar.

Esma Platnumz na Petit Man siku ya ndoa yao.


“Huwa siongei na Esma mara kwa mara kwani sina sababu sana ya kuwa naye kwa kuwa si mume wala bwana’ngu.
“Pia sijawahi kukwaruzana naye, sasa kama kuna kitu alisema, mimi namtafutia wanawake mumewe basi atakuwa anakosea kabisa,” alisema Wema.

BREAKING NEWZ.... MKE MTARAJIWA APASUA JIPU



Erick evarist
KWELI! Baada ya mitandao mbalimbali kuripoti habari zinazokinzana juu ya tukio la bwana harusi mtarajiwa aliyetajwa kwa jina la Stephano kunaswa kwenye tukio la ujambazi muda mfupi baada ya kumvisha pete ya uchumba mpenzi wake, Happy Merere, bi. Harusi huyo mtarajiwa ameibuka na kuanika ukweli wa mambo, Risasi Jumamosi lina full stori.

Stephano akiwa na mpenzi wake, Happy Merere baada ya kumvisha pete ya uchumba.

Stephano na wenzake watatu walikamatwa Aprili 21, mwaka huu maeneo ya Red Cross jijini Dar akidaiwa kuhusika katika tukio la kumpora fedha Mzungu mmoja raia wa kigeni pale Kinondoni, Dar.
Kwenye tukio hilo, watuhumiwa hao, akiwemo Stephano au mume mtarajiwa wa Happy waliwekwa chini ya ulinzi na jeshi la polisi.

MITANDAO YAANZA
Baada ya tukio hilo kuthibitishwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam na watuhumiwa Salum Mtamwa, Alex Makunga, Mohammed Ally na Stephano Kikindi kushikiliwa kwa uchunguzi zaidi, watu walianza kuripoti tofauti katika mitandao ya kijamii.Kuna ambao walidai watuhumiwa hao ni majambazi kwa vile walikutwa na bunduki mbili lakini kuna wengine walidai ni vibaka kwa kuwa hawakukutwa na silaha yoyote.

WENGINE WANADAI NDIYO TABIA YAKE
Wadau wengine kwenye mitandao ya kijamii walijiongeza kwa kudai mtuhumiwa ambaye ni mume mtarajiwa wa Happy wanamjua kwamba anajihusisha na ishu za udokozi hivyo tukio hilo si la kwanza kumtokea.

MKE MTARAJIWA AIBUKA
Risasi Jumamosi lilibahatika kuzungumza na Happy ambaye awali alianza kukanusha taarifa ambazo zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii na kudai nyingi hazina ukweli wowote, alisema:
“Wanajiandikia tu mitandaoni, hakuna ukweli wowote. Eti wanasema mchumba‘angu amekutwa na bunduki mbili wakati taarifa nilizozikuta pale Polisi Central zinasema hawakuwa na silaha.”

ASEMA SI JAMBAZI!
“Wala mchumba‘angu hakuwa jambazi kama watu walivyokuwa wanasema mitandaoni, jalada nililolikuta polisi lilikuwa limeandikwa UNYANG’ANYI na si ujambazi kama wengi walivyokuwa wanavumisha, mimi nimekwenda mwenyewe polisi nikaoneshwa.”

Stephano anayetuhumiwa kwa ujambazi.

KUMBE WAMEJUANA KITAMBO
Katika aya nyingine, Happy alizungumzia uhusiano wake na mumewe mtarajiwa huyo na kusema walifahamiana miaka mingi lakini hawakuwa wakiishi pamoja.“Mimi nimejuana naye miaka mingi iliyopita lakini hatukuwa tukiishi pamoja, yeye anakaa Dar, mimi nipo nyumbani kwa wazazi wangu, Iringa.”

NI MTU WA KUSAFIRI
“Hata hivyo, mimi mwenyewe nyumbani nilikuwa sikai sana, nilikuwa mtu wa kusafiri maana nina biashara zangu, hata yeye tulikuwa tunaonana mara chache.”

KAZI YA MTARAJIWA WAKE
“Tangu nimemjua mtarajiwa wangu alikuwa anafanya kazi ya ufundi wa magari pamoja na udalali wa magari, sikuwahi kusikia wala kumuona anajihusisha na wizi wa namna yoyote. Nashangaa eti watu wanadai ni mzoefu wa matukio ya wizi.”

ADAI NI MARAFIKI
“Wale watu aliokamatwa nao mchumba wangu ni marafiki zake, sasa huenda alijikuta amejumlishwa kwenye tukio ambalo halimhusu. Watu wanazungumza tu pasipo kuwa na ushahidi wowote, mimi mchumba wangu namjua sijawahi kumuona na viashiria vyovyote vya wizi,” alisema Happy.

Stephano na wenzake waliponaswa kwenye tukio hilo.


WAZAZI WACHANGANYIKIWA
Happy alizidi kuweka wazi kuwa, ameumizwa na tukio hilo kwani limewagusa wazazi wake kiasi cha kuwafanya wachanganyikiwe.“Huwezi amini, wazazi wamechanganyikiwa, wanaelezwa vitu vya uongo kuhusu mtarajiwa wangu inaniuma kwa sababu yanayoongelewa kwenye mitandao hayana ukweli, ila ngoja tusubiri vyombo vya sheria vifanye kazi yake na wote waliosema uongo wataumbuka,” alisema Happy.

TUKIO LA PETE
Februari, mwaka huu, Happy alivishwa pete na mchumba wake huyo nyumbani kwao Iringa ambapo mipango ikienda sawa, wawili hao wanatarajiwa kufunga ndoa hapo baadaye mwaka huu (Mungu akipenda).

NAY WA MITEGO, SHAMSA MKE NA MUME!




Musa Mateja

Mara baada ya kuelezwa kwamba wapo kwenye uhusiano wa kimapenzi huku wenyewe wakidanganya wana ‘projekti’, hatimaye majirani wamefichua kuwa mwigizaji Shamsa Ford na mwanamuziki Emmanuel Elibariki ‘Nay’, sasa wanaishi kama mke na mume.

Mwigizaji Shamsa Ford na mwanamuziki Emmanuel Elibariki ‘Nay’ wakizungumza jambo.

Baada ya kutonywa ‘mchapo’ huo, gazeti hili liliwadamkia nyumbani kwa Nay maeneo ya Kimara-Korogwe jijini Dar na kumkuta Shamsa akiwa na kanga moja.Mwanahabari wetu, baada ya kufika nyumbani hapo mishale ya asubuhi alikuwa bega kwa bega kuwafuatilia ambapo alifanikiwa kugundua kwamba wawili hao sasa wanaishi kama mume na mke.

Habari zilizopatikana zilidai kwamba, kwa sasa Shamsa hana muda mwingi wa kukaa nyumbani kwake kwani asilimia tisini kama si mia moja kabisa, anautumia kukaa na Nay nyumbani hapo.Mara kadhaa mwandishi wetu amekuwa akifika nyumbani hapo na kumkuta Shamsa akipika na kupakua huku akiwa na kanga moja huku wenyewe wakiitana mke na mume na kuoneshana mahaba motomoto.

...Wakipozi kimahaba.

“Kwani tatizo lipo wapi? Siwezi kufanya siri tena, sisi tupo kwenye uhusiano wa kimapenzi kama unavyotuona, nimeamua kumchagua Nay kwa kuwa anajua kupenda na kuthamini,” alisema Shamsa alipohojiwa na paparazi wetu.
Alipoulizwa Nay kulikoni ‘kumficha’ Shamsa nyumbani kwake, alifunguka:

“Yeah! Kwa sasa hakuna project tena, hapa ni mapenzi kwa kwenda mbele, sipendi kuwazungumzia wengine, napenda kuangalia uhusiano wangu upo vipi kwa sasa, ninampenda Shamsa.”

...Wakipata msosi.

Nay na Shamsa walianza uhusiano huo mara baada ya mwanamuziki huyo kudai kwamba alimnasa mpenzi wake, Siwema akiwa na mwanaume ndani ya sita kwa sita hivyo kuamua kuachana naye moja kwa moja na kujikuta akiangukia kwa mwigizaji huyo.

A WONDER STORY CLICK TO READ.........'Right' Reasons to Get Married





This is a very important question and sadly, I don't think many people actually ask themselves this question until it's too late.

Lets talk about the "right" reasons to get married:
You share common beliefs about life and marriage.
You are capable of working out differences respectfully.
You can respect each other even when you disagree.
You accept each other for who you are and are willing to support them towards their goals.
You love each other without conditions (having the right weight, education, quid pro quo.)
You feel loved and supported by their family and friends.
You have each other's back and are willing to protect and defend each other when needed.
You are not expecting the other person to "make you happy."
You are interested in sharing and building a life together.
You can tell the person you love what you need and want without manipulation or guilt.
You know you can be vulnerable with each other without judgment or criticism.

If you are uncomfortable about talking about money, sex, time, goals and family concerns with your potential spouse, before you get married.... the situation will not improve once you are married.


This is just something to keep in mind. Get into healthy conversation habits before you make the commitment official. This practice will greatly improve the quality and longevity of your relationship.

Remember, just because you love someone doesn’t mean that you have to marry them. Love is important in marriage, but compatibility is a requirement in order for two people to live a long healthy life together.

I’ve experienced many couples who still loved each other, but love was not enough to remove all of the things that were left unsaid or hidden from their spouse.

If you can’t discuss important issues within your partnership, how will the two of you survive anything and everything that comes your way?

In the next episode, we will discuss the wrong reasons to get married.

If you are avoiding having a difficult conversation with someone and would like to know where to start, you can check out my online course entitled,

AMANDA ACHARUKIWA KISA NGOMA


MWANDISHI WETU

MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Tamrina Poshi ‘Amanda’ amefunguka kuwa baada ya kukanusha kuwa hana ugonjwa wa Ukimwi, mpenzi wake amemcharukia kweli akihoji kwa nini akanushe kama hana?

Mwigizaji wa sinema za Kibongo, Tamrina Poshi ‘Amanda’.

Akizungumzia tukio hilo, Amanda alisema baada ya gazeti la Ijumaa la wiki iliyopita kuripoti akimchana shabiki aitwaye Joel ambaye aliandika mtandaoni kuwa mwigizaji huyo anatumia vidonge vya ARV ili kuongeza nguvu za kuishi, ndipo mchumba wake akacharuka.

“Baby alicharuka kweli akadhani labda pengine ni kweli wakati mimi nimepima na majibu yangu ni mazuri, nilimuelewesha kwamba nilimchamba yule shabiki ambaye aliropoka tu bila ushahidi, nashukuru alinielewa na sasa tuko poa,” alisema Amanda.

WEMA AKUBALI WAGANGA 26 KUMTIBU




KUFUATIA tatizo la kushindwa kupata ujauzito alilonalo msanii maarufu Bongo, Wema Sepetu, hivi karibuni waganga wapatao 26 kutoka sehemu mbalimbali nchini walijitokeza na kuomba kuunganishwa na staa huyo ili wamtibu.

Msanii maarufu Bongo, Wema Sepetu.

Waganga hao wa tiba asilia pamoja na madaktari kutoka hospitali mbalimbali kwa nyakati tofauti walililipigia simu gazeti hili na kueleza kuwa, wanashangaa kuona Wema anakosa amani wakati wao wanaweza kumtibu na kuweza kuitwa mama kama wenzake.

“Unajua wapo wanawake ambao wanakosa amani kwa mambo ambayo hawastahili, hili la Wema kutopata mtoto linatibika, mpeni namba yangu kisha anitafute,” alisema mmoja wa wataalam hao aliyeomba jina lake lisiandikwe gazetini.
Katika kujua Wema anapokeaje ofa aliyopewa na waganga hao, alitafutwa na alipopatikana alikubali mara moja kutibiwa tatizo alilonalo lakini akatoa angalizo.

“Kuna watu wengi sana ukiacha ambao wamejitokeza kwenu, mimi nina meseji zaidi ya 400 ambazo nimetumiwa kwenye namba yangu ya WhatsApp na simu kibao nimepigiwa watu wakijitolea kuja kushughulikia tatizo langu, kiukweli kabisa nipo tayari. “Lakini ni vizuri wakati naanza kutibiwa tayari nikawa na mwenza wangu ambaye tutakuwa tumekubaliana na pale tatizo litakapoisha, iwe rahisi kuzaa mara moja,” alisema Wema.a

ZITTO SPIDI 120




Na Elvan Stambuli
MWENDO wa Kiongozi Mkuu wa Alliance for Change and Transparency (ACT) Wazalendo, Zitto Zuberi Kabwe (pichani) umetafsiriwa kuwa ni wa spidi 160 kutokana na kujawa wasikilizaji katika mikutano yake anayofanya kwenye mikoa mbalimbali nchini.

Kiongozi Mkuu wa Alliance for Change and Transparency (ACT) Wazalendo, Zitto Zuberi Kabwe.

Zitto ameshafanya mikutano katika Mikoa ya Ruvuma, Njombe, Morogoro, Shinyanga na Mwanza na mikutano yake imekuwa ikihudhuriwa na wananchi wengi, hivyo kutumia mwanya huo kugawa kadi za chama chake.
Alipohojiwa na gazeti hili kuhusu hali hiyo ya kujaza watu, Zitto alisema mwendo wa chama chake ni kama moto wa pumba ambao ukiwa unauangalia kwa juu, utadhani umezimika lakini ukiingiza mguu, unaungua.
“Sisi tunafanya kazi usiku na mchana ili kupata wanachama ili uchaguzi mkuu ukifika tupate wabunge wa kutosha,” alisema Zitto aliyewataka wananchi kujiandikisha muda ukifika pale Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) itakapowafikia kuwaandikisha.
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa alipoulizwa kama spidi 160 anayokwenda nayo Zitto haiwezi kuwa tishio kwa chama chake, alisema Chama cha ACT Wazalendo hakiwezi kukitisha chama chake hata kidogo.
Dk. Slaa aliongeza: “Chadema tumeijenga kuanzia ngazi za chini kwa miaka mingi, hatumuogopi yeyote. Dk. Slaa, Mbowe na timu nzima tumezunguka Tanzania nzima kijiji kwa kijiji, hivyo hakuna mtu yeyote atakayekuwa tishio kwetu.”
Akizungumzia Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), alisema imekuwa ikilalamikiwa kuhusiana na kuchelewa kuletwa kwa mashine za mfumo wa Biometric Voters Registration ( BVR), lakini dosari ya msingi katika suala la BVR ni serikali kushindwa kutoa fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa hivyo.
Dk. Slaa alisema Agosti 30 na Septemba 8, mwaka jana, viongozi wa vyama vya siasa nchini walikutana na Rais Jakaya Kikwete na wakajadiliana masuala kadhaa likiwamo la uandikishaji wa Daftari la Wapiga kura kwa kutumia mfumo mpya wa BVR na kukubaliana kuwa mambo ambayo siyo ya kikatiba na yasiyo ya lazima yasifanyike kwanza katika kipindi hiki ili kupunguza gharama.
Dk. Slaa ambaye amerejea hivi karibuni kutoka Marekani, alisema miongoni mwa mambo waliyoyaomba yasifanyike kwanza ni kura ya maoni kwa ajili ya Katiba Inayopendekezwa kwa kuwa siyo jambo la kikatiba, lakini katika hali ya kushangaza serikali ikatangaza tarehe ya kufanyika kura ya maoni licha ya kuwapo makubaliano hayo.
“Rais Kikwete alikubali na kupendekeza kuahirishwa kura ya maoni hadi baada ya uchaguzi mkuu ili kuokoa fedha ili zitumike kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu, lakini hilo halikuzingatiwa,” alisema.
Aliongeza kuwa hadi sasa serikali imetumia fedha nyingi sana kufanya kampeni kwa ajili ya kura ya maoni na cha kushangaza ni kuwa serikali ndiyo inayofanya kampeni badala ya wananchi .
Dk. Slaa alisema wamebaini kuwa kuandikisha wapiga kura kwa kutumia BVR ni mbinu inayofanywa na serikali kwa sababu kuna maeneo ambayo wananchi hawataandikishwa na ndiyo maana wameanza maeneo ambayo ni ngome za Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“Tunataka kuwaambia kuwa tumeshtukia na tunatoa rai kwa Rais Kikwete, nchi hii ni muhimu kuliko yeye, nchi ni muhimu kuliko CCM na kuliko Chadema, hata siku moja upinzani hauwezi kuleta vurugu, vurugu zitaletwa na serikali yenyewe inayotaka kulazimisha mambo yake,” alisema.

CHADEMA NUSURA WAMUUE CHENGE




Na Mwandishi Wetu
Kimenuka! Wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mjini Bariadi, Simiyu, juzi almanusra wayakatishe maisha ya mbunge wa jimbo hilo, Mheshimiwa Andrew Chenge (pichani) baada ya kuvamia msafara wake, hali iliyolazimu risasi zitumike kumuokoa.


Mh. Andrew Chenge

Kwa mujibu wa habari zilizotua kwenye dawati la Uwazi Mizengwe, tukio hilo la aina yake, lilitokea mishale ya saa moja kasoro za jioni, Jumatano ya Aprili 22, 2015 kwenye eneo maarufu la Mwisho wa Lami zilipo ofisi za Chadema wakati Chenge na wafuasi wake wakirejea kutoka kwenye mkutano wa hadhara.
“Yaani ni Mungu tu, hivi sasa tungekuwa tunazungumza mengine kuhusu Mheshimiwa Chenge, wafuasi wa Chadema wangemuua,” alisema shuhuda wa tukio hilo aliyezungumza na gazeti hili kwa sharti la kutoandikwa jina lake gazetini na kuongeza:
“Unajua siku hiyo kulikuwa na mikutano miwili ya hadhara, mmoja wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) uliofanyika eneo la Isanga na kuhutubiwa na Mheshimiwa Chenge na mwingine wa Chadema uliohutubiwa na John Mnyika na Heche.
“Mikutano yote iliisha salama na wafuasi wa Chadema wapatao 2,000, wakawasindikiza viongozi wao kwenda kwenye ofisi za Chadema zilizopo Mwisho wa Lami, kandokando ya Barabara ya Maswa- Lamadi,” alisema shuhuda huyo na kuendelea kuongeza kuwa walipofika kwenye ofisi hizo, waliendelea kuimba na kushangilia na kutawanyika mpaka barabarani.
“Ghafla msafara wa Chenge ukafika eneo hilo huku muziki ukisikika kwa sauti kubwa ndani ya gari moja, wafuasi wote wa Chadema wakiwa wameshika mawe wakauzingira na kuanza kuzomea. Mara Chenge na wafuasi wake wakateremka chini, hapo ndipo kiliponuka.
“Mtu mmoja aliwaamrisha wafuasi wa Chadema kuanza kuwapiga mawe watu wote, akiwemo Chenge, kukatokea bonge la mtiti, Chenge na wenzake wakawekwa ‘mtu kati’ na kutaka kushushiwa kichapo.

MILIO YA RISASI
“Ghafla ikasikika milio ya risasi tatu, watu wote wakatawanyika huku wengine wakikanyagana na kuwapa mwanya Chenge na wenzake kukimbilia kwenye magari yao na kutokomea kusikojulikana, yaani ilikuwa kama filamu ya mapigano vile, aisee,” alisema shuhuda huyo.


Baada ya kupata habari hizo, Uwazi Mizengwe liliwatafuta Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika na Mwenyekiti Mstaafu wa Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha) John Heche kutaka kujua kilichotokea.
Kwa mujibu wa Mnyika, wao walikuwa kwenye ofisi za Chadema lakini ghafla walivamiwa na msafara wa Chenge ukiwa kwenye magari zaidi ya sita huku wakiwa wanapiga muziki kwa sauti kubwa na kuanza kufanya vurugu kabla ya mtu mmoja kwenye msafara huo kuchomoa bastola na kufyatua risasi.

“Ni kweli, ilikuwa ni baada ya mkutano mkubwa viongozi wa Chadema, walisindikizwa na wananchi mpaka kwenye ofisi zetu, Chenge na wenzake wakaamua kuja jirani na ofisi hizo na kufyatua risasi kuwatawanya wananchi,” alisema Mnyika na kumtaka mwandishi awasiliane na Heche ambaye ndiye aliyeenda kuandikisha maelezo kituo cha polisi.
Uwazi lilimtafuta Heche kwa njia ya simu na alipopatikana, alitoa maelezo ambayo hayatofautiani na Mnyika.


“Chenge na wafuasi wake walituvamia ofisini kwetu na kuanza kuleta fujo, ghafla tukashangaa wanatufyatulia risasi, ikabidi wafuasi wa chama chetu wakimbie kuokoa maisha yao,” alisema Heche na kuendelea kueleza kuwa baada ya tukio hilo, walikwenda kutoa taarifa Kituo cha Polisi Bariadi na kupewa RB yenye namba BAR/RB/1195/2015.
“Cha ajabu tulipofika kituoni, tulimkuta Chenge na wafuasi wake nao wamekuja kutoa taarifa,” alisema Heche.

CHENGE SIMU YAKE VP?
Uwazi Mizengwe halikuishia hapo, lilimtafuta Chenge ambaye muda wote simu yake haikuwa ikipatikana hewani. Likaamua kumtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, ACP Gemini Mushi ambaye alikiri kutokea kwa tukio hilo.

ASEMAVYO RPC
“Taarifa zilizopo ni kwamba Mheshimiwa Chenge na wenzake walikuwa wakitoka kwenye mkutano halali walioufanya eneo la Isanga, sasa wakati wanarudi wakapita kwenye ofisi za Chadema zilizopo Mwisho wa Lami ambapo wafuasi wa Chadema waliwavamia na kusababisha vurugu kubwa.
“Katika kujihami, mtu mmoja aliyekuwa kwenye msafara wa Chenge aitwaye Ahmed Ismail alifyatua risasi tatu hewani, ndipo wakapata upenyo wa kukimbia baada ya wafuasi wa Chadema kutawanyika.
“Mkanganyiko uliopo ni kwamba CCM wanasema Chadema ndiyo waliowavamia, Chadema nao wanasema CCM ndiyo waliowavamia, hivyo hali ni tete. Tunaendelea kulichunguza tukio hilo,” alisema Kamanda Gemini na kuongeza:
“Wanasiasa wajifunze kupambana kwa hoja wawapo kwenye majukwaa ya siasa lakini siyo kupigana kwa mawe au bastola.”
Kamanda huyo aliongeza kuwa baada ya kufanya uchunguzi, walibaini kwamba bastola iliyotumika, ilikuwa ikimilikiwa kihalali na Ahmed na kwamba hakukuwa na mtu yeyote aliyejeruhiwa.

MAMA KANUMBA, MAMA LULU KIMENUKA!




Mwandishi wetu
Taarifa zilizotua kwenye dawati la gazeti hili zinadai kuwa, wale wamama wa mjini ambao walikuwa mashosti hadi kufikia hatua ya kusema ni kama ndugu, mama wa aliyekuwa staa wa Bongo Movies, marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa na mama wa mwigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’, Lucresia Karugila, sasa kimenuka!

Mama wa mwigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’, Lucresia Karugila.

DALILI KUWA PAKA NA CHUI
Chanzo chetu cha kuaminika kilidai kuwa, dalili za wawili hao kuelekea kugeuka kuwa paka na chui zilianza muda mrefu lakini hali ikazidi kuwa mbaya Siku ya Kumbukumbu ya Kifo cha Kanumba, Aprili 7, mwaka huu alipokuwa akitimiza miaka mitatu kaburini.

CHANZO NI LULU
Ubuyu ulidai kwamba, siku ya kumbukumbu ya kifo cha Kunumba, Mama Kanumba alimtuhumu Lulu kutotoa ushirikiano na kufikia hatua ya kutoa maneno makali zaidi yaliyomkera mama Lulu.



Mama wa aliyekuwa staa wa Bongo Movies, marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa.

MAMA KANUMBA NA SMS MBAYA KWA MAMA LULU
Ilidaiwa kwamba, siku ya kumbukumbu ya kifo cha Kanumba, mama Kanumba alimtumia mama lulu sms mbaya ya kejeli (kuiandika hapa siyo busara) ndipo mama Lulu ‘alipofyumu’ na kuona kwa hali hiyo bora kama mbwai na iwe mbwai.“Ile sms mama Kanumba alimtumia mama Lulu siku ile (Aprili 7) majira ya saa 11:00 alfajiri.

HAIKUWA YA KIUNGWANA
“Kwa kweli ilikuwa meseji mbaya mno. Alikuwa akimuagiza mama Lulu amuamshe Lulu kwa ajili ya kwenda kaburini kwa Kanumba lakini haikuwa ya kiungwana.“Hata hivyo, ukweli mama Lulu alitumia busara kwa kutomjibu lakini akadhamiria kuchukua hatua za kisheria,” alidai mtoa ‘ubuyu’ huyo.Enzi za ushosti wao.

Ilizidi kudaiwa kwamba, wakati mama Lulu akitafakari sababu ya shosti wake huyo ambaye walikuwa wakitembea mjini kama kumbikumbi kumtumia sms hiyo, akashangaa kusoma tena kwenye gazeti mama Kanumba akimpa vipande vyake Lulu, jambo lililozidi kumchefua mama Lulu.

KUBURUZANA KORTINI?
“Kimsingi hali ni mbaya sana sasa hivi, inavyoonekana mama Lulu kamchoka mama Kanumba na anataka kuchukua hatua zaidi ikiwemo kuburuzana kortini,” alidai sosi huyo.

MAMA LULU AFUNGUKA
Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, gazeti hili lilimtafuta mama Lulu ambapo alipopatikana alikiri kupokea ujumbe na kwamba hali ni mbaya sana.“Nimeumizwa sana na sms ya mama Kanumba lakini siwezi kuwapa kwa sababu nataka kuifanyia kazi,” alisema mama Lulu.

Mwigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’.

MAMA KANUMBA VIPI?
Kwa upande wake mama Kanumba aliendelea kusisitiza kuwa yeye ataendelea kumlilia mwanaye na hana mpango na familia hiyo ya Lulu.“Mimi kwa upande wangu nitamlilia mtoto wangu mpaka siku ya kufa kwangu lakini kinachoniuma ni Lulu kufanya sherehe ya mdogo wake siku ya kumbukumbu ya mwanangu.

“Jamani hata kama mtu ana roho gani, hawezi kufanya hivyo,” alisema.
Alipoulizwa kuhusu sms aliyomtumia mama Lulu na kwamba mama huyo yupo mbioni kumchukulia hatua za kisheria hakuwa tayari kuzungumza chochote.
Newer Posts Older Posts
© Copyright Bongo Mirror | Designed By BONGOJAMII.COM
Back To Top