Loading...

AJALI YA MOTO KICHANGA CHAOKOA FAMILIA!

KICHANGA kinachokadiriwa kuwa na umri wa miezi nane, wiki iliyopita kiliiokoa familia yake kuteketea kwa moto, baada ya kuamka usiku na kulilia kunyonya, kitendo kilichomshtua mama yake aliyebaini nyumba yao ilikuwa ikiungua, huko Kibamba Lungwe jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya nyumba iliyoungua.
Akisimulia tukio hilo, mama wa kichanga hicho, Asha Mohamed, alisema alishtuka baada ya mtoto kuanza kulia akitaka kunyonya, alipoamka ndipo akaona mwanga mkali juu ya paa, hali iliyomlazimu kuamka na kwenda kumgongea Abuu ili kutafuta njia ya kutoka,” alisema mama huyo akiongeza kuwa sebuleni, moto ulikuwa umetapakaa.

Kijana Abuu Masoud (15), baada ya kuamshwa, alionyesha ujasiri na upendo mkubwa kwa kujitoa mhanga kuwasaidia wadogo zake watatu waliokuwa wamelala katika moja ya vyumba vya nyumba hiyo.
Baada ya kuingia katika chumba hicho, alifanikiwa kumtoa mtoto mmoja.
Watoto walionusulika kuteketea kwa moto.
“Nilipofungua mlango wa sebuleni nikaona moto na moshi mwingi sana, roho iliniuma sana kwani chumba cha pili kulikuwa na wadogo zangu watatu wamelala, nikaamua kuvaa ujasiri na kujitosa katika chumba kile na kufanikiwa kutoka na mtoto mmoja, wakabaki wawili,
baada ya kurudi ndani nikapata wazo la kuzima Mean switch, nilipoenda kuishika ikaniangukia kichwani kwani ilikuwa imeshaungua, ndiyo nikaungua na kushindwa kuwatoa waliobakia, ingawa baadaye kuna msamaria mwema mmoja alijitokeza na kuja kubomoa mlango na kuwatoa wengine,” alisema kijana huyo.
....Kitanda walichokuwa wamelala.
Mama wa mtoto mchanga alifanikiwa kutoka pasipo kudhurika.
Aidha baba mwenye nyumba hiyo, Khalfani Maketemo, ambaye wakati nyumba yake inaungua yeye na mkewe walikuwa hospitali alikokuwa amelazwa, anadai chanzo cha moto huo ni shoti iliyoanzia kwenye bati na anaamini ni kutokana na kuunganishwa vibaya kwa waya unaopitisha umeme kutoka kwenye nguzo kwenda kwenye nyumba.
Wakizungumza na mwandishi wetu baadhi ya majirani walisema; “Uunganishwaji wa umeme ni wa kubabaisha, waya unagusana na bati jambo ambalo ni hatari kama waya utachubuka na mvua kunyesha’’.Familia hiyo kwa sasa haina sehemu ya kujisitiri nyumba nzima imeteketea.

KIJANA AUAWA NA KUTELEKEZWA KARIBU NA KAMBI YA FFU







Kijana ambaye hakufahamika jina anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 30 hadi 35 amekutwa ameuawa na mwili wake kutelekezwa katika eneo la kambi ya Polisi Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) kata ya Nshambya mkoani Kagera.


Mwili huo uligundulika majira ya saa sita mchana baada ya watu waliopita katika eneo hilo kuuona ukiwa umelazwa karibu na moja ya shamba lililopo mtaa wa Bunkango eneo la kambi hiyo ya Polisi.


Mpekuzi ilishuhudia mwili huo ulioanza kuharibika ukiwa umevuliwa nguo zote ukiwa bado haujaondolewa katika eneo hilo la tukio.

Mwili huo ulikuwa na majeraha maeneo ya usoni kiasi cha kushindwa kutambulika kirahisi.

Akizungumza na waandishi wa habari waliofika katika eneo hilo, Kaimu Mtendaji wa kata ya Nshambya, Christian Ngaiza, alisema alipata taarifa za tukio hilo kutoka kwa dereva wa bodaboda kuwa kuna mtu ameuawa lakini wananchi wanaogopa kutoa taarifa Polisi.


Ngaiza, alisema baada ya kupata taarifa hiyo aliamua kwenda eneo la tukio majira ya saa saba mchana na kutoa taarifa ya tukio hilo Polisi.

Aidha, alisema baada ya kubaini mwili huo, alianza uchunguzi na kuhoji wananchi wa mitaa yote mitatu ya eneo hilo endapo wana taarifa za mtu yeyote aliyepotea ambapo ilibainika hakukuwa na mtu aliyepotea.

Mkazi wa Mtaa wa Migera, Joyce Nuru, akizungumzia tukio hilo, alisema alipata taarifa za kukutwa kwa maiti huyo, akiwa nyumbani kwake ambapo majira ya saa sita mchana wanafunzi walipita na kumueleza kuwa kuna mtu amekufa maeneo ya mnara.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera ambaye pia ni mpelelezi wa makosa ya jinai mkoani humo, Gilles Mroto alisema tukio hilo amelisikia na ametuma timu ya maofisa wa Polisi kwenda eneo la tukio kufanya uchunguzi.

Hata hivyo, mwili huo haukuweza kutambulika na hivyo kuzikwa na Manispaa ya Bukoba katika makaburi ya Kyebitembe

cr : Jamvi la Habari Tanzania

Kaseja kupandishwa tena kizimbani february 22



Kipa wa Yanga, Juma Kaseja kupitia kwa wakili wake, Samson Mbamba, jana amesomewa shtaka lake kwa mara ya kwanza la kuvunja mkataba kwenye Mahakama ya Kazi.

Kesi hiyo itaunguruma tena Februari 12 na Yanga wanataka Kaseja awalipe Sh340 milioni ikiwa ni ada ya usajili, ambayo ni Sh40 milioni pamoja na fidia ya Sh300 milioni, ambazo ni gharama za usumbufu wa kuvunja mkataba, kumhudumia na kutunza kiwango chake kwa kipindi chote alichokuwa Yanga.

Yanga inawakilishwa na mwanasheria wao, Frank Chacha, ambaye alifungua kesi hiyo Ijumaa iliyopita na ameliambia gazeti hili kuwa wamefikia uamuzi huo ili iwe fundisho kwa wachezaji wengine kuheshimu mikataba yao.

Kaseja aliingia kwenye mgogoro na uongozi wa Yanga baada ya Novemba 11 mwaka jana, kuandika barua ya kuvunja mkataba na klabu hiyo baada ya kukiuka makubaliano ya mkataba kati yao, akishinikiza kulipwa Sh20 milioni za usajili alizokuwa anaidai klabu hiyo.

Kaseja kupitia Kampuni ya Mbamba Advocate, iliandika barua ya kuvunja mkataba na klabu hiyo kwa kile ilichoeleza kuwa amekuwa akisugua benchi.

Pia, uongozi wa Yanga umekiuka makubaliano baina ya pande mbili ambazo hadi Januari mwaka jana walitakiwa kummalizia ada yake ya usajili Sh20 milioni, lakini hata hivyo, haikufanya hivyo hadi alipowasilisha barua ya kuvunja mkataba.

Akizungumza na gazeti hili, Wakili wa Kaseja, Samson Mbamba alisema: “Tutasimama kizimbani, hakuna shida, wala hatubabaishwi na lolote, naamini mteja wangu ana haki zote, mbivu na mbichi zitajulikana.”

Kwa upande wake, kipa huyo wa zamani wa Simba, Kaseja, alisema hana la kusema kwa sasa na kila kitu amekiacha mikononi mwa wakili wake

Kipa wa Yanga, Juma Kaseja kupitia kwa wakili wake, Samson Mbamba, jana amesomewa shtaka lake kwa mara ya kwanza la kuvunja mkataba kwenye Mahakama ya Kazi.

Kesi hiyo itaunguruma tena Februari 12 na Yanga wanataka Kaseja awalipe Sh340 milioni ikiwa ni ada ya usajili, ambayo ni Sh40 milioni pamoja na fidia ya Sh300 milioni, ambazo ni gharama za usumbufu wa kuvunja mkataba, kumhudumia na kutunza kiwango chake kwa kipindi chote alichokuwa Yanga.

Yanga inawakilishwa na mwanasheria wao, Frank Chacha, ambaye alifungua kesi hiyo Ijumaa iliyopita na ameliambia gazeti hili kuwa wamefikia uamuzi huo ili iwe fundisho kwa wachezaji wengine kuheshimu mikataba yao.

Kaseja aliingia kwenye mgogoro na uongozi wa Yanga baada ya Novemba 11 mwaka jana, kuandika barua ya kuvunja mkataba na klabu hiyo baada ya kukiuka makubaliano ya mkataba kati yao, akishinikiza kulipwa Sh20 milioni za usajili alizokuwa anaidai klabu hiyo.

Kaseja kupitia Kampuni ya Mbamba Advocate, iliandika barua ya kuvunja mkataba na klabu hiyo kwa kile ilichoeleza kuwa amekuwa akisugua benchi.

Pia, uongozi wa Yanga umekiuka makubaliano baina ya pande mbili ambazo hadi Januari mwaka jana walitakiwa kummalizia ada yake ya usajili Sh20 milioni, lakini hata hivyo, haikufanya hivyo hadi alipowasilisha barua ya kuvunja mkataba.

Akizungumza na gazeti hili, Wakili wa Kaseja, Samson Mbamba alisema: “Tutasimama kizimbani, hakuna shida, wala hatubabaishwi na lolote, naamini mteja wangu ana haki zote, mbivu na mbichi zitajulikana.”

Kwa upande wake, kipa huyo wa zamani wa Simba, Kaseja, alisema hana la kusema kwa sasa na kila kitu amekiacha mikononi mwa wakili wake

YANGA KUMPANDISHA KIZIMBANI JUMA KASEJA



Baada ya Uongozi wa Klabu ya Yanga kutangaza kuachana na aliekuwa mlindamlango wake Juma Kaseja na baadae kumfungulia mashtaka katika Mahakama ya kazi , hatimaye mlind amlango huyo sasa anatarajia kusomewa mashtaka yanayomkabili February 12 mwaka huu.
Hatua hiyo ilikuja kufuatia Kaseja kudai alipwe fedha zake za usajili zilizokuwa zimesalia na kutaka kuvunja mkataba wake , lakini baadae Klabu hiyo ilimuingizia pesa hizo katika akaunti yake bila kumpa taarifa na kupelekea kuwepo kwa mgogoro baina ya pande hizo mbili.
Mkuu wa Idara ya Sheria ya Klabu hiyo FRANK CHACHA ameiambia mtandao huu kwamba wamepokea samasi inayomtaka mlindamlango huyo kufika Mahakamani hapo kwa ajili ya kesi hiyo
Newer Posts Older Posts
© Copyright Bongo Mirror | Designed By BONGOJAMII.COM
Back To Top